Lindi na vivutio vyake vya kitalii visivyotumika ipasavyo
2006-05-11
Namsembaeli Mduma
Watalii wengi hufika nchini kwa ajili ya kujionea vivutio mbalimbali wakiwemo wanyama, na kuchangia pato la taifa.
Kwa upande mwingine wanyama hao wamekuwa tatizo kubwa kwa wakazi wa maeneo ya karibu na walipohifadhiwa. Mwandishi wetu Namsembaeli Mduma aliyekuwa katika ziara ya Waziri Mkuu, Bw. Edward Lowassa mkoani humo anaelezea zaidi.
Mkoa wa Lindi una eneo la Kilomita za mraba 67,000. Kati ya hizo 18,000 ni hifadhi ya Selous.
Eneo hilo kama linavyojulikana kwa lugha ya kigeni Selous Game Reserve ndilo pori kubwa duniani lililowekwa chini ya urithi wa dunia na UNESCO.
Pori hili lina wanyama wengi na baadhi yao wamo katika hatari ya kutoweka duniani. Wanyama hao ni pamoja na tembo, faru, mamba na mbwa mwitu. Pori hili limetenga karibu hekta 800 kwa ajili ya vitalu vya kuwinda na Watalii ambao pia hufanya utalii wa picha.
Njia zinazotumiwa na watalii hao kufika katika eneo hilo ni pamoja na barabara kutoka Dar es Salaam kupitia Utete na ile ya ndege ambayo huishia kwenye viwanja vyake.
Katika wilaya ya Kilwa kuna pori la ukubwa wa kilomita za mraba 50. Pori hili ni hifadhi inayopendekezwa na linajulikana kama mto Nyange.
Umuhimu wa pori hili ni viboko wengi idadi inayofikia 450 katika bwawa la mto huo. Wanyama wengine wanaopatikana hapo ni chui, tembo, nyati, simba, kongoni na jamii ya ndege na nyani.
Mbali na mapori hayo, yapo ya wazi na yale ambayo hayakutengwa kwa ajili ya hifadhi za Wanyamapori au Misitu.
Kutokana na taarifa ya sekta hiyo ya maliasili kwa Waziri Mkuu, maeneo haya ya wazi ndimo wananchi huwinda wanyamapori kwa ajili ya kitoweo na kujistarehesha.
Kuna mapori mengine yaliyotengwa kwa ajili ya jamii vijijini na yapo kando kando ya Hifadhi ya Selous.
Wananchi hushirikishwa katika uhifadhi na papo hapo hufaidika na mapato ya uwindaji wa wanyama unaofanywa na wenyeji na Watalii.
Vijiji vya wilaya ya Liwale vimetengewa maeneo ya aina hii.
Mpango huo unategemewa kuanzishwa katika wilaya ya Kilwa pia.
Lakini, pamoja na watalii kuvutiwa na wanyamapori, wamekuwa wakiharibu mazao mashambani na hivyo kusababisha hasara kubwa.
Mfano wanyama kama nguruwe, tembo, boko na nyani ndio hasa wanaoelezwa kuwa kero kubwa katika maeneo ambayo wanavijiji wapo mmoja mmoja au wapo katika sehemu za mbali mbali kwenye maeneo makubwa.
Ukiachilia wanyama hao, wapo wakali ambao nao wanaelezewa kuwa tatizo kubwa kwa watu na mifugo yao. Wanyama hao ni kama simba na wengineo.
Maelezo ya maofisa wa wanyama pori kwa Waziri Mkuu yanasema kuwa wanyama hawa wanapata urahisi wa kuwaingilia watu vijijini kutokana na ulinzi mdogo wa askari wa Wanyamapori, kufuatia uchache wao na ukosefu wa zana za kisasa zakutosha.
Miaka ya 1980, mkoa wa Lindi ulikuwa na askari wa wanyama pori takriban 40 lakini sasa imeporomoka hadi kufikia 25 tu. Uchache huo ndio unaosababisha jitihada za kuwadhibiti wanyama hao waharibifu kukwama.
Kutokana na takwimu za mwaka 2004, watu 30 waliuawa na simba katika mkoa huu na wilaya zilizoathirika zaidi zilikuwa Liwale na Lindi.
Watu na mifugo hushambuliwa zaidi na wanyama hao wakali nyakati za kiangazi ambapo kuna kuwa na ukame wa maji na malisho.
Hali hiyo inawasukuma wanyama hao wa porini kuingia katika makazi ya watu hasa ya karibu nao na kuleta tafrani au kuua kabisa.
Kwa kuwa utalii ni moja ya hazina kubwa ya mkoa huu, jitihada mbalimbali hufanywa na Serikali kuhakikisha haipotei, uhifadhi wa mazingira unapewa kipaumbele zaidi, kwa kuwaelimisha wananchi juu ya upandaji wa miti na utunzaji wa ile mioto ya asili.
Kuna fukwe za bahari kama vile Mitema na Mchinga katika wilaya ya Lindi na Jimbize, Masoko Pwani na Mto Kiswere wilayani Kilwa.
Vivutio vingine ni Majengo ya kale ya kihistoria wilayani Kilwa kama vile magofu ya Kilwa Kivinje, Kilwa Kisiwani, na Siongo Mnara. Magofu haya yalijengwa na Waswahili, Waarabu na Wareno kati ya karne ya 14 na 19.
Mapango mengine ni ya Nang'oma wilayani Kilwa ambayo ndimo Wamatumbi walijificha wakati wa vita vya Maji-Maji kati ya Wajerumani na Wamatumbi hao.
Katika pango hili, kuna mapango madogo madogo ambamo walizikwa watu waliouawa vitani.
Siku hizi mapango haya yanahifadhiwa na jamii inayoyazunguka.}
Katika kijiji cha Tenganduru wilayani Lindi kunapatikana mabaki ya mnyama aliyeitwa Dinosaur aliyeishi miaka 65-208 milioni iliyopita.
Mabaki mengine ya wanyama hao yalichukuliwa na kupelekwa Berlin katika jumba la Makumbusho kabla ya Tanganyika kupata uhuru wake.
Mbali na wanyamapori, mkoa huo umejaliwa misitu mikubwa ya asili aina ya miombo yenye ukubwa wa Hekta 4, 272,000 na misitu ya kupandwa aina ya Pine Hekta 2000 ambayo ipo kwenye miinuko ya Tarafa ya Rondo.
Misitu ya mikoko imeenea katika eneo la pwani ya Bahari ya Hindi kwa Hekta 26,500.
Hii inafanya mkoa wa Lindi kuwa wa tatu hapa nchini kwa kuwa na eneo kubwa la misitu hiyo baada ya mikoa ya Tabora ambao una hekta 53,600,000 na ule wa Rukwa wenye Hekta 4,900,000.
Kati ya Kilomita za mraba 42,720 za misitu ya asili ya miombo, kilomita za mraba 5,893 ni misitu ya hifadhi ambapo asilimia 87 iko cini ya Serikali Kuu wakati asilimia 13 ipo chini ya Serikali za Mitaa (Halmashauri za wilaya).
Eneo lililobaki ni la kilomita za mraba 36,827 ambazo ni maeneo ya misitru isiyohifadhiwa.
Msitu wa Rondo wenye Hekta 2000 ni msitu pekee wa miti laini kwenye mkoa huu. Msitu huu pamoja na mikoko yote ina hadhi ya hifadhi.
Tunapozungumzia misitu hatuna budi kuzungumzia upandaji miti. Kutokana na takwimu za mkoa huo upandaji wa miti katika wilaya za Ruangwa, Nachingwea, Kilwa, Liwale na Lindi ulikuwa kama ifuatavyo; kuanzia Julai 2002 hadi Juni 2003 na Julai 2003 hadi 2004.
Kilwa ilipanda miti 320,900 ambapo miti 312 ilipona, mwaka uliofuata ilipanda miti 500,000 na ilipona 330,000.
Lindi ilipanda miti 662,250 na ikapona 660,436. Mwaka uluofuata ilipanda miti 1,000,000 na ikapona 630,000.
Kadhalika wilaya ya Nachingwea kwa miaka ya mwanzo ilipanda miti 600,000 ambapo ilipona 542,815.
Kipindi kilichofuata ilipanda miti 1,000,000 na ilikua 750,000.
Ruangwa ilipanda miti 1000,000 kipindi cha kwanza na ikaota 500,000 wakati miaka iliyofuayta ilipanda miti 1000,000 tena na iliyokua ilikuwa 500,000.
Pamoja na kukua kwa sekta hii mkoani humo, inakumbwa na vikwazo mbalimbali kama vile uvunwaji wa miti usio halali, kutoonwa na jamii kuwa ni zao la kilimo na biashara kama mengine.
Hata hivyo,sekta hiyo ya misitu inamwelekeo wa kupunguza umasikini kwa asilimia 50 ifikapo mwaka 2005 na kuufuta kabisa ifikapo mwaka 2025.
|
|
Le attrazioni turistiche di Lindi non sono sfruttate come si deve
2006-05-11
Namsembaeli Mduma
Molti turisti vengono nel paese per vedere le diverse attrazioni, fra cui gli animali, e contribuiscono alle entrate del paese.
D'altra parte questi animali costituiscono un grande problema per gli abitanti delle zone vicine alle riserve. Lo spiega il nostro corrispondente, Namsembaeli Mduma, che ha accompagnato il Primo Ministro Sig. Edward Lowassa, nella sua visita della regione.
La regione di Lindi ha una estensione di 67.000 km quadrati. Di questi 18.000 costituiscono la riserva Selous.
Questa zona nota in lingua inglese come Selous Game Reserve, ? una delle grandi foreste del mondo dichiarate patrimoni mondiali dall'UNESCO.
Questa foresta ha molti animali e alcuni di loro sono in pericolo di estinzione. Si tratta di elefanti, rinoceronti, coccodrilli e lupi (licaoni). Da essa circa 800 ettari sono stati adibiti a riserva di caccia e per i turisti che fanno turismo fotografico.
Le vie usate dai turisti per arrivare nella zona sono la strada da Dar es Salaam che passa per Utete e gli aerei con i relativi aeroporti.
Nel distretto di Kilwa c'? una foresta dalla grandezza di 50 chilometri quadrati. Questa foresta ? una interessante riserva ed ? nota come fiume Nyange.
L'importanza di questa foresta sono i circa 450 ippopotami che vivono negli stagni del fiume. Altri animali presenti qui sono leopardi, elefanti, buffali, leoni, antilopi e famiglie di uccelli e scimmie.
Oltre a queste foreste vi sono zone deserte e quelle non destinate a riserve di animali selvaggi.
Dalle informazioni su questo settore delle risorse naturali fornite al Primo Ministro, in queste zone deserte sono i cittadini a cacciare gli animali selvaggi per alimento e per divertimento.
Altre foreste sono riservate alle comunit? dei villaggi, sono quelle lungo la Riserva di Selous.
I locali partecipano alla conservazione e contemporaneamente beneficiano del ricavato dalla caccia fatta dai cittadini e dai turisti.
I villaggi del distretto di Liwale sono stati ricavati da zone di questo tipo.
Si prevede di realizzare lo stesso progetto anche nel distretto di Kilwa.
Ma, oltre ad attrarre i turisti, gli animali rovinano i raccolti dei campi e quindi causano gravi perdite.
Per esempio sono soprattutto animali come cinghiali, elefanti, ippopotami e scimmie la grande calamit? nelle zone in cui gli abitanti sono isolati o sono sparsi in una grande area.
Oltre a questi animali, ve ne sono anche di feroci che costituiscono un vero problema per gli uomini e i loro allevamenti. Si tratta di leoni e simili.
Dalle informazioni fornite al Primo Ministro da funzionari per gli animali risulta che questi animali hanno facile accesso agli abitanti del villaggio per la inadeguata vigilanza delle guardie [forestali], a causa della loro scarsezza e della insufficienza di attrezzature moderne.
Negli anni '80 il distretto di Lindi aveva circa 40 guardie forestali, ma ora sono scese a sole 25. E' questa scarsit? che causa il fallimento degli sforzi di controllare gli animali dannosi.
Secondo i dati del 2004, 30 persone sono state uccise dai leoni in questa regione e i distretti pi? colpiti sono stati Liwale e Lindi.
Le persone e gli allevamenti sono assaliti da questi animali soprattutto durante la stagione calda, quando c'? scarsit? di acqua e cibo.
Questa situazione spinge gli animali selvati ad entrare nelle zone abitate, soprattutto quelle pi? vicine, e creano confusione o uccidono.
Poich? il turismo ? una delle grandi risorse di questa regione, il Governo fa diversi sforzi per assicurarsi che la conservazione dell'ambiente riceva una priorit? maggiore, insegnando ai cittadini a piantare alberi e a conservare quelli spontanei.
Vi sono spiagge come Mitema e Mchinga nel distretto di Lindi e Jimbize, Masoko Pwani e fiume Kiswere nel distretto di Kilwa.
Altre attrattive sono le Antiche Costruzioni storiche nel distretto di Kilwa, come i resti di Kilwa Kivinje, Kilwa Kisiwani e Siongo Mnara. Questi sono resti di costruzioni swahili, arabe e portoghesi dei secoli che vanno dal 14 al 19.
Altre grotte sono quelle di Nang'oma nel distretto di Kilwa in cui Matumbi si nascosero durante la guerra Maji Maji fra i tedeschi e i matumbi.
In queste grotte vi sono piccoli antri in cui sono state seppellite le persone uccise durante la guerra.
Attualmente queste grotte sono conservate dalla comunit? circostante.
Nel villaggio di Tenganduru, del distretto di Lindi, vi sono i resti di un [animale chiamato] dinosauro vissuto 65-208 milioni di anni fa.
Altri resti di questi animali sono stati presi e inviati al Museo di Berlino prima che il Tanganyika ottenesse la sua indipendenza.
Oltre che di animali selvaggi questa regione ? piena di grandi foreste spontanee di "myombo" [un albero la cui corteccia viene usata per fare vestiti, e si svolge l'iniziazione delle ragazze] della grandezza di 4.272.000 ettari e foreste di pini di 2.000 ettari piantati sulle colline della provincia di Rondo.
Foreste di rizoforee si estendono nella zona costiera dell'Oceano Indiano per 26.500 ettari.
Questo fa della regione di Lindi la terza nel paese per estensione di foreste dopo le regioni di Tabora con 53.600.000 ettari e quella Rukwa con 4.900.000.
Dei 42.720 chilometri quadrati di foreste spontanee di "myombo", 5.893 chilometri quadrati di foreste sono protette, di cui l'87 percento ? sotto il controllo del Governo Centrale, mentre il 13 percento dipende dal Governo locale (Consiglio Distrettuale).
La rimanente zona ? di 36.827 chilometri quadrati e non ? protetta.
La foresta di Rondo di 2.000 ettari ? una foresta di alberi caratteristici della regione. Questa foresta assieme a tutte le rizoforee ? stata dichiarata una riserva.
Parlando di foreste dobbiamo parlare della piantagione di alberi [non locali]. I dati relativi a questa regione la piantagione di alberi nei distretti di Ruangwa, Nachingwea, Kilwa, Liwale e Lindi ? avvenuta da luglio 2002 a giugno 2003 e da luglio 2003 al 2004.
Kilwa ha piantato 320.900 alberi di cui 312 [312.000?] hanno attecchito, l'anno seguente ha piantato 500.000 alberi e 330.000 hanno attecchito.
Lindi ha piantato 662.250 alberi, di cui 660.436 hanno attecchito. L'anno seguente ha piantato 1.000.000 alberi e 630.000 hanno attecchito.
Inoltre il distretto di Nachingwea il primo anno ha piantato 600.000 alberi di cui 542.815 hanno attecchito.
Nel periodo seguente ha piantato 1.000.000 e 750.000 hanno attecchito.
Ruangwa ha piantato 1.000.000 nel primo periodo, di cui 500.000 hanno attecchito mentre negli anni seguenti ha piantato di nuovo 1.000.000 e quelli che hanno attecchito furono 500.000.
La crescita di questo settore nella regione ? colpita da diversi ostacoli come la caccia di contrabbando e il fatto che la popolazione non sente queste foresete come prodotti agricoli e commerciali.
Tuttavia questo settore delle foreste ha l'obiettivo di far diminuire la povert? del 50 percento ento il 2005 e eliminarla completamente entro il 2025.
(
Nino Vessella)
|